NAMNA YA KUFANYA UPEKUZI (SEARCH) KISHERIA

Anaandika Bashiri Yakubu

Kupekua( search)   ni  tendo  ambalohufanywa  na  mamlaka  za  usalama  katika  maeneo   mbalimbali   hasa  katika makazi   yawatu.  Mbali  na  makazi  ya  watu  kupekua  pia  kwaweza  kufanyika   katika    magari, treni,  na  vyombo  vyote  vya  usafiri  zikiwemo  ndege  na  meli.  Pia  kupekua  kwaweza kufanywa  kwa  mtu  kwa  maana  kuwa  mtu    kama  mtu  naye anaweza  kupekuliwa(search). Iwe  mifukoni  au  wapi  lakini  mtu  naye  hupekuliwa. Kwa  jina  la  mtaani  kupekua  hujulikana  kwa  jina  la  kupiga  sachi. Hivyo  basi  kupekua  na  kupiga  sachi   ni  kitu  kilekile. Mbali  na  kuwa  upekuzi  waweza kufanyika  sehemu nyingi  kama  tulivyoona makala  haya   yatagusa  upekuzi  katika maeneo    ya nyumbani kwa maana  kwenye   makazi  au  maofisi. Suala  la upekuzi  kwa  ujumla  wake  huongozwa  na  Sura  ya  20, Sheria  ya  Mwenendo  wa  Kesi  za  Jinai  kama  ilivyofanyiwa  marekebisho  2002  na  wakati  mwingine  Sheria  ya  Jeshi  la  Polisi Sura  ya  322.1.SABABU  ZA  KUPEKUA.Kisheria  sababu  za  kupekua  lazima  iwe  ni  katika  kutafuta  ushahidi ambao  utawezesha  kupatikana  kwa  ukweli  wa  jambo  fulani  ambalo  lipo  katika  ngazi  za upelelezi  katika  mamlaka  fulani.  Hauwezi  kufanyika  upekuzi  nyumbani  kwa  mtu  kwa  lengo  jingine  na  hilo  likitokea   basi  itakuwa  ni   kinyume cha  sheria. Sehemu inayopekuliwa ni  lazima  kuwepo  na  tetesi   au  uhakika  wa  kuwa eneo  hilo  upo  ushahidi  unaotafutwa  kwa  ajili   kuanzisha,kuendeleza  au  kukamilisha upelelezi  fulani.  Kwa  hiyo  sababu  kubwa  ya  upekuzi(search)  ni kutafuta  ushahidi. Hakuna  upekuzi  kwa  ajili ya sababu  binafsi.2.    NANI  HUTAKIWA  KUFANYA  UPEKUZI (SEARCH).Askari  polisi  anayo  mamlaka  ya  kufanya  upekuzi  katika  nyumba  yamtu.  Nyumba  yaweza  kuwa  ya  makazi  au ya  biashara  kama  duka,mgahawa, hoteli,  nyumba  za  wageni,  na  vyuoni  na  mashuleni. Zaidi  maafisa  wengine  kama   taasisi  ya  kuzuia  na  kupambana  na  rushwa   au  wale    wa  mamlaka ya  chakula  na  dawa  ( TFDA) n.k.nao  wanaweza  kufanya  upekuzi. Isipokuwa  maafisa  hawa wenginekama   mamlaka  ya  chakula  na  dawa  wanaruhusiwa  kufanya  upekuzi  katika  yale  maeneo  yanayohusu  ile  kazi  yao  tu,  kwa  mfano   dukani  kukagua bidhaa  basi  na  si  kuingia  mpaka   chumbani  kwa  mtu. Hata  hivyo  wanashauriwa   kuambatana  na afisa  wa  polisi mara  zote wanapoamua  kufanya  upekuzi.3.  HAIRUHUSIWI  KUFANYA  UPEKUZI  USIKU  BILA  KIBALI  CHA MAHAKAMA.Kifungu  cha  40  cha  Sheria  ya  Mwenendo  wa  Kesi  za  Jinai  kinasema  kuwa   hati  ya  upekuzi  inaweza kutolewa na  kutekelezwa  siku  yoyote  na  inaweza  kutekelezwa  kati  ya  muda  kuchomoza  au  kuchwa  kwa jua lakini  mahakama  inaweza  kwa  maombi  ya  afisa  polisi  au  mtu  mwingine  yeyote  ambaye  imeelekezwa  kwake kumruhusu  kutekeleza  muda  wowote.   Katika  tafsiri  ya  kifungu  hiki  kuna  mambo   mawili  ya  msingi.Kwanza  tunaona  kuwa upekuzi  kawaida  unatakiwa  ufanyike  siku  yoyote  kati  ya  jua  kuchomoza  na  jua  kuchwa. Jua  kuchwa  ni    jua  kuzama. Kawaida  muda  wa  jua  kuchomoza  maeneo  mengi  ya  Tanzania  ni  kuanzia  Sa   12  za  asubuhi  na  ,maeneo  mengine  saa 11  za  asubuhi.  Na  muda  wa  jua  kuzama   maeneo  mengi  ni  kati  ya saa  12  za  jioni  hadi  saa  moja  jioni. Kwahiyo  huo  ndio  muda   wa  kawaida  ambao  upekuzi  unatakiwakufanyika    kwenye  nyumba  za  watu. Kimsingi  ni  muda  wa  mchana( day time).Pili, tafsiri  inayofuata   katika  kifungu  hicho  ni pale  kinaposema  kuwa  kwa  kibali  maalum  cha  mahakama  upekuzi  unaweza  kufanyika  muda  wowote. Hapo  juu tumeona  upekuzi  unatakiwa  kufanyika  katika  muda  maalum  ambao  kimsingi  ni  asubuhi  mpakajioni (mchana). Hapa  sasa tunaona kuwa   upekuzi  unaweza  kufanyika  muda  wowote ikiwemo  usiku  wa  manane  lakini  hii  itakuwa  kwa  kibali  maalum  cha  mahakama.  Kwahiyo  tunaona  wazi  kuwa  ili  upekuzi  ufanyike   usiku   yapaswa  kuwepo  kibali  cha  mahakama  ambacho  kimeruhusu  kufanya  hivyo vinginevyo  upekuzi  wote   hutakiwa  kufanyika  masaa  ya   mchana. Kwa  maana  hii  unapogongewa  usiku  na  askari  wanaojitambulisha  kuhitaji  kufanyaupekuzi  kwako basi kabla  ya  kuruhusu  zoezi  hilo  kufanyika  omba  kuona  kibali  cha  mahakamahata  kupitia  dirishani kwanza. ACHA KUNYANYASWA, CHUKUA  HATUA.

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

KILOMETERS KUTOKA DAR ES SALAAM KWENDA MIKOANI

MAANA HALISI YA NENO KATERERO