MAJIBU RAHISI UWAPO MBELE YA MAHAKAMA
UKIWA MAHAKAMANI UNAJIBU MASWALI JARIBU KUTOA MAJIBU KAMA IFUATAVYO
( 1 ) Kama unahojiwa na Wakili mahakamani usijibu bila kutafakari alichokuuliza.( 2 ) Wakili asikuogopeshe kwa ukalianapokuuliza kwani ukali hulenga kuleta paniki na kukusahaulisha ulichopanga kusema.
( 3 ) Usilazimishe kujibu kitu ambacho hukijui ni bora kusema sijui kuliko kulazimisha kujibu.
( 4 ) Penda sana kujiamini kwakuwa kujiamini hupunguza uwezo wa Yule anayekuuliza, hata awe Jaji/Hakimu.
( 5 ) Jitahidi kupata ushauri wa wanaojua sheria kwa kila hatua unayopiga katika kesi.
( 6 )Kama we ni shahidi hakikisha unajadiliana vya kutosha na Yule unayemtolea ushahidi kabla hamjaingia mahakamani.
( 7 )Usipaniki kiasi cha kutoa neno lolote la kashfa ,kejeli, au tusi mahakamani unaweza kuongeza kosa la kuidharau mahakama.
( 8 )Katika kesi ya jinai usikubali kosa haraka kabla hujajua kitaalam kosa hilo linaundwa na nini(vipengele vya kosa).
( 9 )Kama hukuelewa vizuri kosa ulilosomewa ni bora kukaa kimya, kwakuwa ukikaa kimya unaandikiwaumekataa kosa.
( 10 )Kanuni ya sheria ni kuwa, Ni kazi ya aliyekushitaki kuthibitisha kwa ushahidi kuwa umetenda kosa na si kazi yako kuthibitisha kuwa haujatenda kosa.
( 11 )Katika kesi ya jinai msikilize kwa makini anayekushitaki na hakikisha unapata lolote lenye kutia shaka katika maelezo yake na iambie mahakama shaka hilo hii ni kwasababu huwezi kuwa na hatia kama kuna shaka katika maelezo.
(12)Kama ulitenda kosa katika harakati za kujitetea usidhuriwe iambie mahakama kuwa ulitenda kosa ukijilinda(self defence) inaruhusiwa, hata kama uliua waweza kuachiwa.
( 13 )Kama ndugu yako hana akili tinmamu na ametenda kosa iambie mahakama.Hii ni kwasababu kutokuwa na utimamu wa akili ni kinga inabidi aachiwe lakini hatarudi nyumbani atapelekwa vituo vya wasio na akili.
( 14 )Inakubalika na ukaachiwa huruukisema kuwa ulilazimishwa kutenda kosa kama kweli ulilazimishwa.
( 15 ) )Inakubalika na ukaachiwa huru kusema kuwa sikuwa eneo la tukio wakati likitokea kama kweli haukuwapo.
( 16 )Kama kosa ni kupita taa nyekundu ikiwaka barabarani,swali lako kwa shahidi traffic lilenge kumbana kama sehemu aliyokuwa amesimama alikuwa na uwezo wa kuangalia vizuri na kutambua rangi za taa. Mfn. jua kali linawaka yeye ameuonaje mwanga wa taa kutoka mbali.
( 17 )Ukipewa nafasi ya kumhoji shahidi muhoji maswali mafupi. Mfn. ulikaa upande wa pili barabara, si ndio, jua kali lilikuwa linawaka , si ndio, ulifanya kazi ya kuangalia magari mengine pia si ndio, na mbele kulikuwa na miti si ndio, sasa kama hali ilikuwa hivyo uliwezaje kuona taa nyekundu ikiwaka wakati nakatiza.
(18 )Ukipewa nafasi ya kumhoji shahidi wako uliyemleta katu usimuulize swali ambalo mlikuwa hamjalijadili na hivyo hujui atatoa jibu gani.
( 19 ) Kama wanaokushtaki wanashahidi na unamjua kuwa kunakipindi aliwahi kuchangnyikiwa au kufanya tukio lolote la uhalifu kabla, ni nafasi nzuri kuhoji uwezo na uadilifu wake mpaka aaminike kwa anayoyatolea ushahidi leo..........ITAENDELEA
Comments
Post a Comment