Posts

Showing posts from April, 2017

Kwa video hii ni ishara tosha ya vita kuu ya tatu ya dunia, hebu tazama wewe mwenyewe kujionea video hii

Image
Video. Kwa Hali ilivyo sasa Katika ulimwengu huu hivi ni viashiria vya vita kuu ya tatu ya dunia ni vyema kila mmoja wetu aombe Mungu atuepushe na balaa hili.

HARAKATI ZA HAKI ZA BINADAMI NA MAHAKAMA ZA TANZANIA

From Yona Fares JAJI MWALUSANYA VS HUKUMU YA KIFO. Mwaka 1994 katika mahakama kuu mkoani Dodoma mbele ya Jaji Mwalusanya J, watu wawili Mbushuu Mnyaroje na Kalai Sungula walikutwa na hatia ya kosa la mauaji ambapo waliua mtu na kupora mifugo yake. Walikutwa na kosa la mauaji ya kukusudia (murder) kinyume na kifungu cha 196 cha Penal Code Cap 16.  Walitakiwa kupewa hukumu ya kifo kwa mujibu wa kifungu cha 197 cha Penal Code, Kunyongwa mpaka kufa kwa mujibu wa kifungu cha 26 cha Penal Code. Kabla jaji hajatoa hukumu wakili wa Mbushuu na Sungula wakili Rweyongeza aliibua hoja kuhusiana na adhabu ya kifo kwamba hukumu ya kifo ni kinyume kabisa cha katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ya 1977 ibara 13(6)(d) na (e) kwa maana kwamba hukumu ya kifo ni ya kikatili,ya mateso, inayotweza utu wa mtu na isiyo ya kibinadamu. Wakili Rweyongeza alienda mbali zaidi na kusema hukumu ya kifo ni kinyume cha katiba ibara ya 14 inayotoa haki ya kuishi, kwa hoja hizo aliiomba mahakam...

HII NDIO HOTUBA YA MWISHO ALIYOITOA COLONEL MUAMARY GADAFI KABLA YA KIFO CHAKE YANI INASIKITISHA NA KUTIA UCHUNGU

HOTUBA YA MWISHO YA GADAFFI KWA WA AFRICA GADAFFI ANAANZA HIVI: "Kwa jina la Mwenyezi Mungu (Allah), Mungu mpaji, na mwenye rehema.... Kwa miaka takribani 40 ama ilikuwa zaidi sikumbuki. Nachokumbuka ni kuwa nilifanya kila nilichoweza kuwapa watu wangu nyumba, hospitali na shule. Na kila walipohisi njaa niliwapa chakula. Niliifanya Benghazi kutoka jangwa kuwa ardhi nzuri ya kilimo. Nilisimama imara dhidi ya Ronald Regan (Rais wa zamani wa Marekani), alipomuua binti yangu niliyemuasili. Alikua anajaribu kuniua mimi lakini akamuua yule binti yatima masikini. Niliwasaidia kaka na dada zangu waafrika fedha kupitia AU. Nilifanya kila nililoweza kuwafanya watu wangu waelewe maana halisi ya demokrasia; ambapo watu wa tabaka la chini niliwapa madaraka. Lakini hawakuridhika. Hata aliyekuwa na nyumba ya vyumba kumi, nguo mpya, na fanicha nzuri, hakuridhika. Alihitaji zaidi. Kwa jinsi walivyokuwa wabinafsi walihitaji zaidi. Hivyo wakawaambia Marekani kuwa wanataka "demokr...